Karagwe forum Karagwe forum Author
Title: WANAWAKE WAMETAKIWA KUNYONYESHA WATOTO WAO KWA KIPINDI CHA MIEZI 6
Author: Karagwe forum
Rating 5 of 5 Des:
Wazazi na walezi katika manispaa ya BUKOBA mkoani KAGERA wameshauriwa kutambua umuhimu kuwanyonyesha watoto wao maziwa ya mama katika  k...

Wazazi na walezi katika manispaa ya BUKOBA mkoani KAGERA wameshauriwa kutambua umuhimu kuwanyonyesha watoto wao maziwa ya mama katika  kipindi cha miezi sita hadi miaka miwili ili kuepuka magonjwa yasiyo ya lazima..

Kauli hiyo imetolewa na mganga mkuu wa manispaa ya bukoba DK HAMZA MUGULA wakati akizungumza na mwandishi wa habari wa FADECO Radio juu ya umuhimu wa kumunyonyesha mtoto .

DK MUGULA ametoa kauli hiyo zikiwa zimebaki siku chache kabla ya maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji nchini.
Amewataka wazazi kutambua kuwa maziwa ya mama ni muhimu hususani kwa watoto  katika kipindi cha  miezi sita kwani  maziwa hayo yanavirutubisho ambavyo vinazuia magonjwa mbalimbali kwa mtoto.


DK MUGULA amezitaja changamoto zinazokabili khali ya lishe kuwa ni kuamini mila na destuli  potofu  watoto kuachishwa kunyonyeshwa mapema pamoja na huelewa mdogo kuhusu  maswala unyonyeshaji.

Hata hivyo katika kukabiliana na changamoto hizo DK MUGULA amesema kuwa wanaendelea kutoa elimu ya unyonyeshaji  na lishe kwa watoto wadogo pamoja na chakula kinachotakiwa kwa wanawake wenye ujauzito na wenye watoto wachanga .


About Author

Advertisement

Post a Comment

 

This Template Is Designed By Jacksay | call 0764 031 242 for this service

Top