Maafisa watendaji wa kata na vijiji na wenyeviti wa
vijiji na vitongoji katika kata zilizopo katika ukanda wa Bushangaro wilayani
Karagwe mkoani Kagera wametakiwa kufuatilia na kupiga marufuku wanunuzi wa
kahawa za magendo ambao tayari wameanza kuzunguka vijijini kwa wakulima kwa
ajili ya kuwalaghai kuwauzia kahawa za magendo.
Wito huo umetolewa na mkuu wa kituo cha polisi Omukarilo
wilayani Karagwe Antony Bupamba wakati akiongea na baadhi ya viongozi wa kata
za Kibondo,Nyakabanga,na Nyakakika wilayani humu.
Bupamba amesema kuwa
tayari wanunuzi wa kahawa za magendo wameshaanza kupita kwa wakulima kwa
ajili ya kununua kahawa mbichi jambo
ambalo ni kinyume na sheria ambapo amesema kuwa ni jukumu la viongozi wa vijiji
kuhakikisha wanapambana na watu wanaofanya hivyo kwa kuwafikisha katika vyombo
vya sheria.
Amesema kuwa watakaemkamata wamfikishe katika kituo cha
polisi na hatua dhidi yake sitachukuliwa ikiwa ni pamoja na kulala ndani kwa
muda wa masaa 24 ili iwe fundisho kwa watu wengine wanaofanya hivyo.
Nao wananchi waliongea na mtandao huu wamekili kuwepo kwa
vitendo vya uuzaji wa kahawa za magendo huku wakijihusisha na vitendo vya
uvunaji wa kahawa mbichi na kuanika chini jambo ambalo wamelitaja kuwa ni
kutofuata ushauari wa wataalamu ambao wanaotoa kila siku.
Hata hivyo wamewataka wananchi kuacha kuitupia lawama
serikali kwani kuzidi kushuka kwa bei ya kahawa kila mwaka ni kutokana na
uvunaji mbovu wa kahawa ambao unasababisha kahawa kutokuwa na ubora.
About Author
The part time Blogger love to blog on various categories like Web Development, SEO Guide, Tips and Tricks, Android Stuff, etc including Linux Hacking Tricks and tips. A Blogger Template Designer; designed many popular themes.
Advertisement

Related Posts
- KAGERA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA VYAFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KUENDELEA KUJIIMARISHA KUWALINDA RAIA NA MALI ZAO25 Apr 20180
Na: Sylvester Raphael Vyombo ya Ulinzi na Usalama Mkoani Kagera vyafanya mazoezi ya ...Read more »
- MBIO ZA MWENGE WA UHURU KATIKA WILAYA ZA KARAGWE NA NGARA PIA HITIMISHO WILAYANI BIHARAMULO MKOANI KAGERA16 Apr 20180
Na: Sylvester Raphael Mwenge wa Uhuru waendelea kuchanja mbuga Mkoani Kagera kwa ku...Read more »
- MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MKOANI KAGERA NA KUANZA UZINDUZI WA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI YA ZAIDI YABILIONI 1216 Apr 20180
Na: Sylvester Rapahel Mwenge wa Uhuru umepokelewa leo April 8, 2018 Mkoani Kagera na...Read more »
- TIMU YA WATAALAM WA UJENZI KUTOKA NCHINI CHINA YAKAGUA ENEO LA UJENZI WA CHUO CHA VETA KAGERA ILI KUANZA UJENZI MARA MOJA16 Apr 20180
Na: Sylvester Raphael Serikali ya Watu wa China yatuma timu ya Wataalam wa Usanif...Read more »
- MKOA WA KAGERA WAVUKA LENGO KATIKA UNDIKISHAJI WA WANAFUNZI AWALI NA DARASA LA KWANZA MWAKA 201816 Apr 20180
Na: Sylvester Raphael Mkoa wa Kagera wavuka lengo la uandikishaji wa Wananfunzi katika madarasa...Read more »
- MKUU WA MKOA KAGERA AAGIZA MKANDARASI KUKAMATWA NA KUFIKISHWA OFISINI KWAKE AKIWA NA PINGU MIKONONI BAADA YA KUITIA SERIKALI HASARA08 Mar 20180
Na Sylvester Raphael Mkuu wa Mkoa wa Kagera aagiza Mkandarasi wa Kampun...Read more »
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.